GEITA GOLD YALAZIMISHWA SARE NA KAGERA SUGAR IKIWA NYUMBANI

Timu ya Geita Gold imeshindwa kupenya mbele ya Kagera Sugar baada ya kulazimishwa sare ya bao moja kwa moja.
Kagera Sugar ilikuwa timu ya kwanza kuona lango la Geita Gold, bao lililofungwa na Abeid Athuman katika dakika ya 34 ya kipindi cha kwanza kabla ya Seleman Ibrahim kuisawazishia Geita dakika ya 73 bao lililodumu hadi dk 90 zinakamilika.
Geita Gold inafikisha alama 2 huku Kagera Sugar akianza leo kuwa na pointi 1 tangu ligi ianze baada ya kupoteza MECHI mbili za awali dhidi ya Azam Fc na Simba sc mechi zilizochezwa jijini Dar es salaam
Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
No comments: