BAADA YA KUTEMWA SIMBA CHRIS MUGALU APATA TIMU MPYA YA MSIMU HUU, LWANGA BADO

Aliyekua mshambuliaji wa Klabu ya Simba SC, Chriss Mugalu (31) amejiunga na timu ya jeshi la anga la Iraq, Al Quwa Al-Jawaiya ambayo inashiriki ligi kuu nchini humo.

Mugalu ambaye ni raia wa Congo DR ni moja ya wachezaji walioachwa na Simba hivi karibuni baada ya pande zote mbili kufikia makubaliani.

Mugalu amesaini kandarasi ya mwaka mmoja kuwatumia wajeda hao wenye maskani yao katika wilaya ya Rusafa, Baghdad.

Wengine waliotemwa pamoja na Mugalu ni Medie Kagere ambaye tayari amesajiliwa na Singida Big Stars na Thadeo Lwanga ambaye bado hajajulikana anakwenda wapi.

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp +255 753 336 000 au +255 625 917 902

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.