YANGA YASHINDWA KUTAMBA MBELE YA AZAM IKIWA NYUMBANI

Klabu ya Yanga leo imelazimishwa sare ya mabao 2 -2 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa ligi kuu NBC uliopigwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Feisal Salum 'Fei Toto' leo anastahili tuzo ya nyota wa mchezo kwa upande wa yanga akiwasaidia wananchi kuondoka na alama moja muhimu

Daniel Amoah aliitanguliza Azam FC kwenye dakika ya 24 baada ya mpira wa kichwa kumpita Diarra

Yanga ilikwenda mapumziko ikiwa nyuma ya goli 1-0 ambapo mkufunzi wa Yanga Nasreddine Nabi, alifanya mabadiliko wakati wa mapumziko kwa kuwaingiza Feisal Salum na Djuma Shaban katika nafasi ya Dickson Job na Denis Nkane

Mabadiliko hayo yaliisaidia Yanga kurejea mchezoni kwenye kipindi Feisali akiisawazishia Yanga goli dakika 56 ya kupitia shuti la nje ya 18

Changamoto ya krosi bado inaendelea kuitesa Yanga kwani mpira wa kona uliopigwa na Azam FC kwenye dakika ya 64 uliwasaidia kufunga bao la pili kupitia kwa Ndoye

Hata hivo Yanga ilirejea tena mchezoni baada ya kupata mkwaju wa penati Bernard Morisson akiangushwa kwenye eneo la hatari penati ambayo haikuwa bahati kwani Djuma Shaban alikosa

Dakika ya 76 wakati wananchi wakiwa katika hali ya kupoteza matumaini, Fei Toto akaachia shuti jingine nje ya 18 lililomshinda golikipa wa Azam Ahmad na kujaa nyavuni goli lililoleta usawa wa bao 2- 2 hadi dk 90 zilipokamilika.

Mchezo wa leo ulikuwa mchezo mgumu sana wenye upinzani mkali ambapo pengine matokeo hayo yanaakisi ugumu wa mpambano huo

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp +255 753 336 000 au +255 625 917 902

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.