TUISILA KISINDA ATUA RASMI DAR KUANZA KAZI NA YANGA

Winga wa Yanga Tuisila Kisinda ametua nchini kuanza majukumu yake katika kikosi cha Yanga

Yanga imemrejesha Kisinda akitokea klabu ya RS Berkane ya nchini Morocco

Mkurugenzi wa mashindano wa klabu ya Yanga Saad Kawemba amesema wamemsajili Kisinda kwa ajili ya kumtumia kwenye mashindano ya ndani na michuano ya kimataifa

Taratibu za usajili wake zilikamilika ndani ya dirisha la usajili ikiwa ni pamoja na kupata ITC yake, Yanga ikimbadilisha na Lazarus Kambole kwa ajili ya Ligi ya ndani

Kisinda pia amesajiliwa kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo awamu ya pili ya dirisha la usajili litafungwa Septemba 15

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp +255 753 336 000 au +255 625 917 902

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.