SOFIA SIMBA ARUDISHWA CCM

Mkutano wa halmashauri kuu ya CCM Taifa umeridhia kumpokea  Kada wa Chama hicho Sofia Simba ambaye alifukuzwa na chama hicho baada ya kubainika kukisaliti chama hicho kwa kumuunga mkono  Edward Lowassa ambaye sasa ni kada wa CHADEMA.

Mwenyekiti wa CCM taifa John Pombe Magufuli amesoma barua ya Sofia Simba kuomba radhi ambapo amesema aliandika barua nyingi za kuomba kusamehewa baada ya kukiri makosa yake na kwamba yeye amekulia ndani ya CCM hivyo hajisikii kuishi nje ya chama hicho.

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp +255 753 336 000 au +255 625 917 902

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.