MAMA YAKE DIAMOND AINGIA BONGO MUVI, MUVI YAKE YA KWANZA KUCHEZA NDIO HII
Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum, mama Diamond alitamba kwenda kimataifa kwenye upande wa filamu kama anavyofanya mwanaye Diamond akiwa ameshiriki katika utayarishaji na uigizaji wa filamu iitwayo Mtepela iliyochezewa huko Kibirizi mkoani Kigoma.
“Nimefanya hiyo filamu na wasanii wa Kigoma, nawajua vizuri lakini kwa sasa siwezi kuizungumzia zaidi,” alisema mama Diamond.
Kwa upande wa mtayarishaji aliyeshirikiana naye aliyejitambulisha kwa jina la Isaya Lazaro almaarufu Zito, alisema mama Diamond mbali na kushiriki katika utayarishaji wa filamu hiyo pia alitoa fedha na ni mmoja wa waigizaji waliofanya vizuri ndani yake.
“Tulimwandalia scene (vipande), akavicheza lakini kabla ya kumaliza alipata safari ya kwenda Afrika Kusini na baada ya kurejea tuendelea kuimalizia”, alisema Zito.
Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi