Flora Mbasha sasa akataa hadi jina


Msanii wa nyimbo za injili Flora Mbasha amesema swala la mahusiano na mapenzi ni ya watu wawili hivyo hataki kuweka wazi juu ya ishu yake ya kudai talaka.
 
Emmanuel Mbasha akiwa na Flora Mbasha kabla ya kuachana

Akiongea kupitia eNEWZ Flora ambaye amesema anataka kuitwa madam Flora kwa sasa kwa kuwa maisha yake anayoyaishi kwa sasa yana amani na furaha hivyo anapendelea kuishi vile apendavyo yeye na kwa sasa hapendi kuongelea kwenye media kwa kuwa maisha yake hayata wanufaisha chochote.


Hata hivyo Madam Flora amesema kwa sasa hajali watu wanayoyaongea juu ya maisha yake na Mbasha kwa kuwa wengi wanaoongea hawamfahamu na wala hawajawahi hata kumshika mkono lakini pia hakusita kumuombea Mbasha kuwa Mungu ampiganie.