IBADA YA UBARIKIO WA WANAFUNZI WA KIPAIMARA YAFANYIKA KATIKA KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA USHARIKA WA EBENEEZER KANISA KUU SHINYANGA.

Leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Usharika wa Ebeneezer kumefanyika ibada njema iliyoambatana na matukio mbali mbali ikiwemo ubarikio wa wanafunzi wa kipaimara,ubatizo wa watoto na watu wazima,kupokea muumini mpya kutoka dhehebu jingine na sakramenti takatifu.


Akihubiri katika ibada hiyo mchungaji na mkuu wa shule ya sekondari ya Mwadui YOHANA NZELU, amesema
“Na itakuwa hata siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana, utawekwa imara juu ya vilima na mataifa yote watauendea makundi makundi. Na mataifa mengi watakwenda na kusema, njooni twende juu yam lima kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu. Naye atafanya hukumu kwa mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu, taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.” ISAYA 2:2-4

Akaendelea kusema “Kuna vitu vilivyomsukuma Isaya kuandika haya hasa alipoangalia mazingira ya jamii inayomzunguka. Ndipo akagundua kuwa watu wamejaa ubinafsi, rushwa,udhalimu na haki imepotea. Watu waliendelea na desturi za ibada zao, pasipo kuweka uchaji wa ibada. Ndipo Isaya anaanza kukemea udhalimu, dhuluma, rushwa akitetea maisha ya wanyonge. Anawakumbusha watu wanaowakandamiza wengine kuwa kuna siku inakuja mwana wa Adamu atakapokuja, kutakuwa na kusanyiko kubwa ambapo mkuu wa haki atonekana akitenda haki kwa wote.Kanisa la leo linapitia zaidi ya haya yaliyoonekana katika kipindi cha Isaya, pengine sasa jamii imeharibika zaidi ya ile ya awali. Kwa sasa watu hatuishi kwa uchaji wa ibada badala yake tunathamini desturi za dini zetu. Mtu anataka aonekane akiwa na bahasha walakini uchaji wa ibada ndani yake umepotea. Hofu ya Mungu imepotea,watu hawamwogopi Mungu. Juzi yametokea maafa Kagera, pande nne za nchi na hata nje ya nchi watu wakishirikiana na serikali wakaamua kuchangia ili kuokoa maisha ya watu, kuwapa msaada wa kurudisha miundo mbinu iliyoharibiwa na tetemeko. Lakini kwa kuwa hofu ya Mungu imepotea, watu wengine wanaamua kufungua akaunti feki ili kijinufaisha kupitia janga hilo, hii ni hatari sana kwa maisha yetu.  Serikali inatangaza kuwa wamama wajawazito,  watoto na wazee watibiwe bure katika hosptali za serikali lakini kwa uroho na tamaa ya mali mtu anaamua kujinufaisha kupitia nafasi hiyo. Unaenda kununua  kilo 50 ya cementi dukani,lakini ukifika nyumbani unakuta kilo ziko 48.
Huu ni udhalimu uliokithiri, hofu imepotea, watu hawamwogopi Mungu. Bwana anakuja katika utukufu wake kuhukumu katika haki, na kila mtu atatoa hesabu ya matendo yake. Na katika ujio huo wale ambao wamejiandaa na kujaa maisha ya toba wao watastahimili na Mungu hataona haya kuitwa Mungu wao, Mungu atusaidie tuishi maisha ya toba.
Hongereni vijana wa kipaimara kwa kufikia hatua hii, sasa mnaenda kukutana na jamii kama hii aliyoiandikia Isaya, nawasihi mwende mkafanikiwe kuwa nuru, chumvi, mkamtumikie Mungu kwa uaminifu. Najua wengine mtakuwa walimu,wengine viongozi, wengine wafanyabiashara, Jitahidini kwenda kutenda haki. Wewe utakayekuwa daktari katende haki,watu wakapate faraja kupitia ninyi. Mkaishi maisha ya toba nay a kumwangalia Mungu daima. Pengine mtakutana na shida, dhiki na mahangaiko, Mungu akawe msaada wenu mkimtegemea yeye siku zote za maisha yenu.
 MUNGU ALIBARIKI NENO LAKE AMEEN!!

Msaidizi wa Askofu na Dean wa kanisa kuu Shinyanga akiendesha ibada ya Ubarikio wa wanafunzi wa kipaimara 

Msaidizi wa Dean kanisa kuu Shinyanga akiongoza watu kuimba wimbo wa kitabuni

 Mwinjirist Elisha Swai akisoma matangazo wakati wa ibada 
Mkristo mpya akipokelewa kuwa mlutheri  kutoka dhehebu la FPCT


ZIFUATAZO NI PICHA ZA MATUKIO YA UBATIZO
Ubatizo ukiendelea 
















ZIFUATAZO NI PICHA ZA MATUKIO YA UBARIKIO WA KIPAIMARA