KAMA WAO YATIKISA! MUGGA MO NA BANDO MC WAACHIA NGOMA KALI MPYA

 MUGGA MO NA BANDO MC WATOA WIMBO MPYA “KAMA WAO” 

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya, Mugga Mo kwa kushirikiana na Bando MC, wameachia rasmi wimbo wao mpya unaoitwa “Kama Wao”, ambao tayari umepokelewa kwa kishindo kwenye mitandao ya kijamii na YouTube.

Wimbo huo umetayarishwa kwa ubunifu mkubwa na maproducer wakali Prez Beatz na Jay Drama chini ya lebo ya @skiasound, huku video ikiongozwa na @iamblaxx, ambaye amefanikisha kuleta muonekano wa kuvutia unaoendana na hadhi ya wasanii hao.

“Kama Wao” ni ngoma inayobeba ujumbe wa kujiamini, ushindi na maisha ya mtaani, ikiwa na midundo ya kuvutia inayomfanya msikilizaji kuurudia mara kwa mara. Mchanganyiko wa flow ya Mugga Mo na uandishi wa Bando MC unazidi kuonyesha kuwa muziki wa Bongo Fleva unaendelea kukua na kuchukua nafasi kubwa.

Mashabiki na wadau wa muziki wanahamasishwa kusikiliza wimbo huo kupitia YouTube kwa kubofya kiungo hiki hapa chini:

Sikiliza Hapa:

Post a Comment

0 Comments