AHUKUMIWA KIFUNGO CHA JELA KWA WIZI WA KUKU NIGERIA

Mahakama ya Jos, mji mkuu wa jimbo la kati mwa Nigeria la Plateau State, imemhukumu mwanaume mmoja kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kuiba kuku.

Hakimu mkazi Daniel Damulak alimhukumu David Akubu mwenye umri wa miaka17- baada ya kukiri kuiba kuku , lakini pia alimpiga faini ya Naira 10,000.

Alimuamuru mshitakiwa kumlipa Naira 5,000 Bi Esther Dazam wa Farin Gada, ambaye alimshitaki kwa wizi huo, na akamtaka akome kufany auhalifu wa aina yoyote ile.

Awali , mwendeshamashitaka katika kesi hiyo, Ibrahim Gokwat, aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa aliiba kuku ya mwanamke , akaipika na kisha kuila na marafiki zake

Post a Comment

0 Comments