WATU SABA WAUAWA NA WENGINE KADHAA WAJERUHIWA KWA MLIPUKO PAKISTAN


Watu saba wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa kufuatia mlipuko uliotokea katika soko moja mashariki mwa Pakistan.

Habari zinasema mlipuko huo ulilenga hoteli moja katika maeneo jirani na mji wa Lahore.

Shambulizi hilo limefanyika wakati ghasia zinazohusishwa na makundi la IS na Taliban zimekuwa zikiongezeka nchini Pakistan, ambapo wiki kadhaa zilizopita takriban watu 130 waliuawa nchini humo katika ghasia.