YANGA YAPIGWA FAINI YA TSH MIL. 1.5, MASHABIKI WASABABISHA

Kamati ya uendeshaji na usimamizi wa ligi kuu Tanzania katika kikao chake cha Agosti 26, 2022 ilipitia mwenendo wa matukio mbalimbali kwenye ligi na kufanya maamuzi

Yanga imetozwa kiasi cha Tsh. 1,000,000/= baada ya mashabiki wake kurusha chupa uwanjani katika mchezo dhidi ya Polisi Tanzania uliopigwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid

Katika mchezo dhidi ya Coastal Union Yanga imetozwa faini ya Tsh 500,000/= kwa kosa la kufanya mabadiliko kwa mikupuo minne badala ya mikupuo mitatu kama inavyoelekezwa kwenye kanuni.

Mwamuzi aliyechezesha mchezo huo Raphael Ikambi ameondolewa kwenye ratiba ya waamuzi kwa raundi tatu baada ya kushindwa kutafsiri sheria

Ni katika tukio la kiuongo wa Coastal Union Mtenje Albano kumfanyia rafu mbaya mlinzi wa Yanga Yannick Bangala

Kamati imewakumbusha wachezaji wote na maafisa wa benchi la ufundi kuzingatia mchezo wa kiungwana Fair Play

Post a Comment

Previous Post Next Post