
Polisi katika eneo la Rabuor Kaunti ya Kisumu wanazuiliwa mwanamume mmoja wa miaka 42 kwa tuhuma za kumnajisi na kumpachika mimba binti wake wa kambo.
Polisi walisema kuwa mshukiwa alikamatwa katika kaunti ndogo ya Kadido baada ya walimu wa mwanafunzi huyo wa darasa la saba kugundua kuwa alikuwa ameanza kudhihirisha tabia zisizo za kawaida.
Kw akuhojiwa, msichana hyo mwenye umri wa miaka 13 alifunga na kupelekwa katika kituo cha afya kilicho karibu ambacho alithibitishwa kuwa na uja uzito wa miezi minne.
Kwa mujibu wa naibu chifu wa kata ndogo ya Kapiyo Amos Odeny, mshukiwa tayari amepinga madai ya kuhusika na unajisi wa mtoto huyo.
“Mtoto huyo amepelekwa katika nyumba iliyo salama. Mwanamume huyo ni baba wa kambo wa msichana. Alioa mamake kama mke wa pili,” Odeny alisema.
Kiambu: Msichana mwenye matatizo ya akili atungwa mimba
Mnamo Juni 16, 2022, TUKO.co.ke iliripoti kuwa familia moja katika kijiji cha Ikuma eneo bunge la Gatundu Kusini kaunti ya Kiambu ilitaka kiongozi mmoja wa kanisa kufungwa maisha kwa tuhuma za kumpachika mimba binti yao mwenye matatizo ya kiakili.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 14 na ambaye alikuwa katika darasa la saba katika shule ya watu wenye changamoto za akili, alilazimika kuacha masomo ili kutunza mimba yake ya miezi mitatu.
Kwa mujibu wa familia, msichana huyo alipewa ujauzito na kiongozi wa kanisa ambaye pia ni kiongozi wa Baraza la Wazee wa Kikuyu katika kijiji hicho.
Mwanamume huyo kwa jina Elikanah Waweru anaripotiwa kuomba familia hiyo kumruhusu binti yao aishi kwake ili amsomeshe kwa kuwa ana uwezo wa kifedha na moyo wa kuimarisha viwango vya maisha.
Familia hiyo ambayo haina uwezo wa kujihakikisha mlo mara tatu kwa siku, ilimkabidhi mwanamume binti yao kwa shukrani, ikitarajia kuwa yuko katika mikono bora na salama.
Wasichokuwa wakijua ni kwamba wanamume huyo alimfanya binti yao kuwa mke wake wa pili na alishiriki naye tendo la ndoa mara kwa mara.
Tags:
habari