
Mahakama umefanya uamuzi huo leo Jumatano tarehe 29, Juni, 2022 kufuatia maombi ya Kibatala ya kuondosha mapingamizi ya awali waliyowaweka kwenye Hati ya kiapo.
Kibatala ameiomba kuondosha mapingamizi hayo ili kupisha usikilizwaji wa shauri hilo kwa kuwa limefunguliwa mahakamani hapo kwa Hati ya dharura.
Jaji Mustapha Ismail amekubali ombi hilo na kuamua kuondoa mapingamizi hayo kabla ya shauri la msingi kuendelea kusikilizwa ambapo amesema kuwa amri ya zuio itaendelea mpaka shauri la msingi litakapofika mwisho.
“Baada ya kusikiliza hoja za Mawakili nimeamua Hati ya mapingamizi ya awali inaondolewa mapingamizi yote hayatataendelea”
Pia Jaji Mustapha amesema kuwa amri ya itaendelea mpaka mwisho wa shauri la msingi.
Wakati huo huo kolamu ya Mawakili imejitambulisha mbele ya Jaji kwa ajili ya kuendelea na shauri hilo.
Tags:
habari