
Kikosi cha Simba kimeonesha kweli kimedhamiria kuibuka na ushindi dhidi ya Al Masry SC katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kesho.
Katika hali isiyo ya kawaida, kikosi hicho kilifanya mazoezi kuanzia majira ya saa moja mpaka mbili usiku wa jana kwenye uwanja wa Boko Vetarani, Dar es Salaam.
Taarifa zinaeleza kuwa wachezaji wapo katika morali nzuri kuelekea mchezo huo utakaopigwa majira ya saa 12 jioni.
Aidha wachezaji Emmanuel Okwi, John Bocco na Haruna Niyonzima wote walijumuika na wenzao kujifua kuelekea mechi hiyo kubwa.
Simba watafanya mazoezi ya mwisho leo kabla ya kuwavaa Al Masry jioni ya kesho.
Tags:
michezo