
Aidha, Rais Dkt Magufuli alielezea baadhi ya changamoto zinazokabili muhimili wa mahakama ambapo alisema kuwa tatizo la rushwa limekuwa likisababisha kukosekana kwa haki kwa atu wanyonge huku kesi nyingine zikicheleweshwa kwa makusudi. Rais Dkt Magufuli amewataka watumishi wa mahakama kuhakikisha wanatoa huduma bila upendeleo.
Baada ya kuzungumza huko, tafrani kubwa ilizuka baada ya mama mmoja kunyanyuka akiwa na kitambaa kilichoandikwa jumbe mbalimbali kuelekea kwa Rais akionyesha kudhulumiwa haki yake huku mahakama na polisi wakihusika.
Hapa chini ni video ya tukio hilo
Tags:
habari