MSHINDI WA KIDATO CHA NNE ATAKA KUWA MWEKEZAJI WA VIWANDA AFRIKA

 
Mshindi wa kwanza kitaifa katika matokeo ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2016 Alfred Shauri amesema ndoto yake ni kuwa mhandisi wa umeme wa viwanda.


Alisema hayo jijini Dar es Salaam alipotembelea ofisi za kampuni ya magazeti ya serikali (TSN) inayochapisha magazeti ya ya DailyNews, SundayNews, Habarileo, Habarileo Jumapili na SportLeo.
 
"Ndoto yangu ni kuwa mhandisi wa umeme wa viwanda ili kutengeza mashine za viwanda, natarajia kuwa mwekezaji wa viwanda afrika," alisema Alfred.
Aliwashauri vijana kutumia mitandao ya kijamii kwa manufaa ya maendeleo.

CHANZO - HABARI LEO
Previous Post Next Post